Timu ya Dodoma Jiji imejipata katika uwanja wake wa nyumbani wa Jamhuri baada ya kuhakikisha wanashinda kila mchezo wawapo hapo.
Dodoma ambayo imecheza na timu ya TRA United jana imefanikiwa kushinda michezo minne katika uwanja huo,sare mbili na huku ikipoteza mchezo mmoja tu katika michezo saba ambayo timu hiyo imecheza uwanjani hapo.

Katika mchezo wa jana ulionza majira ya saa moja usiku Dodoma ilionekana ikizitaka alama zote tatu kutoka kwa TRA kwani timu hiyo ilitawala mchezo ambapo dakika ya 15 ya mchezo huo Faraji Kayanda alifungua ukurasa wa mabao.
TRA nayo ilionekana ikiuta ka mchezo kwa kutaka kusawazisha hata hivyo ndoto yao ilizimwa na mchezaji wa Gadiel Michael ambaye aliongeza bao la pili kwa timu yake hivto kwenda mapumziko Dodoma ikiwa mbele kwa mabao mawili.
Kipindi cha pili kilirejea ambapo dakika ya 55 Edgar William alizidi kudidimiza matumaini ya TRA baada ya kuongeza bao la tatu kwa timu yake ambapo mpaka mchezo unatamatika Dodoma iliibuka na ushindi wa 3-0 hivyo timu hiyo ilipanda kutoka nafasi ya saba hadi ya sdita katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.
[13/02/2026, 09:26:53] Honest Tplb: mkuu



