Tag: #LIGIKUU #NBCPL #AZAM #YANGA #SIMBA #KMC #JKT #MASHUJAA #KENGOLD #DODOMAJIJI #PAMBAJIJI #KAGERASUGAR #SINGIDABLACKSTARS #FOUNTAINGATE #NAMUNGO

YOUNG AFRICANS YAREJEA KILELENI LIGI KUU YA NBC.

TIMU ya Young Africans imeendelea kuonyesha kwanini inaiwakilisha nchi kwenye mashindano ya Afrika baada ya kushinda 3-1 dhidi ya Dodoma Jiji na kukwea hadi nafasi ya kwanza ya msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

Young Africans iliyokuwa ya kwanza kuruhusu bao dakika nne kabla ya kipindi cha kwanza kutamatika kupitia kwa Edgar William haikukata tamaa na zikisalia dakika tatu mchezo kwenda mapumziko ilisawazisha kupitia kwa Laurindo Dilson akitumia mkwaju wa penati baada ya Andy Bikoko kumchezea rafu mchezaji wa Young Africans.

Kipindi cha pili Laurindo aliongeza bao na Prince Dube kupigilia msumari wa tatu na kupeleka furaha kwa ‘Wananchi’ na huzuni kwa ‘wakulima wa zabibu’.

Laurindo Dilson ‘Depu’ amekuwa na kiwango bora kwenye Ligi Kuu ya NBC tangu ajiunge na Young Africans akifunga mabao matatu na kutoa pasi ya bao moja huku akishinda tuzo ya mchezaji bora wa mchezo dhidi ya Dodoma Jiji na kufanikiwa kuifanya Young Africans kurejea kileleni ikifikisha jumla ya alama 22.

Young Africans inaungana na Azam Fc na kuwa timu pekee ambazo hazijapoteza mchezo hadi sasa kwenye Ligi Kuu ya NBC na zikiwa zimeruhusu mabao machache pia (2) huku ‘Wananchi’ wakiongoza kwa kufunga mabao hadi sasa (21).

Mkoani Tanga kwenye uwanja wa Mkwakwani Coastal Union ililazimishwa sare ya bao moja na timu ya KMC ikiwa sare ya pili kwa KMC iliyopoteza michezo nane hadi sasa na ikishika nafasi ya mwisho ya msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

KMC iliyoshinda mchezo mmoja pekee hadi sasa imefanikiwa kufikisha mabao matatu kwenye ligi hiyo ikiwa timu iliyofunga mabao machache hadi sasa huku ikiongoza kwa kufungwa mabao mengi (18).

Sare hiyo inaifanya Coastal Union iliyopoteza mchezo wao uliopita ugenini dhidi ya Namungo kukwea hadi nafasi ya 11 ikifikisha jumla ya alama 10 ikiwa imepata ushindi kwenye michezo miwili pekee.

 

DODOMA JIJI, PRISONS KUUMANA LEO LIGI KUU YA NBC.

TIMU ya Dodoma Jiji itaikaribisha Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC utakaochezwa leo majira ya saa 1:00 usiku kwenye uwanja wa Jamhuri, Dodoma.

Mchezo huo ni muhimu kwa timu zote mbili kwani zinapambana kujinasua ‘mkiani’ Dodoma Jiji ikiwa nafasi ya 15 katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC baada ya kucheza michezo tisa ikishinda mchezo mmoja ,kupata sare minne na kufungwa michezo mitano .

Mchezaji wa Dodoma Jiji Mwana Kibuta

Aidha Dodoma Jiji imeruhusu mabao 10 huku ikifunga mabao matano na kuweza kukusanya alama saba katika michezo hiyo.

Kwa upande wa Tanzania Prisons inashika nafasi 14 katika msimamo ikiwa imecheza michezo saba, ikishinda michezo miwili, sare mbili na kufungwa michezo minne.

Kwa upande wa alama timu hiyo imefanikiwa kukusanya alama saba, ikifunga mabao matatu na kufungwa mabao matano katika michezo hiyo.

AZAM, COASTAL WANA KIKAO LIGI KUU YA NBC LEO.

MATAJIRI wa Chamazi timu ya Azam leo itakuwa na kibarua cha kusaka alama tatu muhimu nyumbani dhidi ya Coastal Union kwenye uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.

Ikiwa na kumbukumbu mbaya ya kuanza mwaka 2026 vibaya baada ya kupoteza kwenye fainali ya Kombe la Mapinduzi dhidi ya Young Africans Azam itavaana na Coastal inayoshika nafasi ya 12 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

Azam inayoshika nafasi ya tisa bado haijapoteza mchezo wowote wa ligi hiyo msimu huu sawa na timu ya Young Africans ambayo pia haijapoteza mchezo.

Tayari Coastal Union imepoteza michezo mitatu msimu huu ikishinda miwili na kutoa sare mitatu ikiwa imekusanya jumla ya alama tisa hadi sasa.

Huu ni mchezo pekee wa Ligi Kuu ya NBC unaopigwa leo baada ya jana timu ya Dodoma Jiji kulazimishwa sare ya bao moja nyumbani na Singida Black Stars.

 

PRISONS WABABE WA MBEYA DABI LIGI KUU YA NBC

Mchezaji wa Mbeya City (kushoto) akichuana na mchezaji wa Tanzania Prisons

TIMU ya Tanzania Prisons imeendeleza ubabe wake katika mchezo wa dabi ya Jiji la Mbeya baada ya kuifunga timu ya Mbeya City mabao 2-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliochezwa Uwanja wa KMC mkoani Dar es Salaam jana Oktoba 21.

Mchezo huo ulianza majira ya saa 10:00 alasiri ambapo timu zote zilikuwa zikipambana kupata alama tatu huku mashabiki wa timu zote mbili wakionekana kushangilia kwa bendi na ngoma zilizonogesha mchezo huo.

Mbeya City kinara wa Ligi Kuu ya NBC alianza mchezo kwa kushambulia sana lango la ‘hasimu’ wake huku Tanzania Prisons ikifanya mashambulizi ya kushtukiza na hadi timu zinaenda mapumzikoni hakuna aliyekuwa ametikisa ‘nyavu’ za mwenzake hivyo kuwapa kazi ya ziada makocha wakati wa mapumziko namna bora ya kujipanga kwa ajili ya kipindi cha pili.

Dakika ya 73 kipindi cha pili Tanzania Prisons ilipata bao la kwanza kupitia kwa Jeremiah Juma na dakika moja baadae Haruni Chanongo aliiongezea bao la pili na kufifisha matumaini ya Mbeya City kubakiza alama zote tatu nyumbani.

Tanzania Prisons wakishangilia

Dakika ya 87 Mbeya City ilipata bao la kufutia machozi kupitia kwa Daniel Lukandamila hivyo mchezo kutamatika kwa Mbeya City kupoteza 1-2 na kuifanya ‘Purple Nation’ kupoteza mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu ya NBC msimu huu.

Mchezaji wa Tanzania Prisons, Jeremiah Juma alitangazwa kuwa mchezaji bora wa mchezo kutokana na kiwango kizuri alichokionyesha ikiwa ni pamoja na kuwafungia ‘Wajelajela’ bao na kuonyesha kiwango kizuri akiisaidia timu yake kushinda.

Jeremiah Juma

Matokeo hayo yanaifanya Tanzania Prisons kupanda hadi nafasi ya tano ikiwa na alama sita huku Mbeya City ikiendelea kushikilia ‘usukani’ wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa na alama saba.

AZAM,JKT

AZAM, JKT HAPATOSHI ISAMUHYO, SIMBA IKIIKARIBISHA NAMUNGO LIGI KUU YA NBC.

MZUNGUKO wa tatu wa Ligi Kuu ya NBC unaendelea leo mkoani Dar es salaam katika viwanja viwili vya Meja Jenerali Isamuhyo na uwanja wa Benjamin Mkapa.

Katika mchezo wa kwanza utakaochezwa Isamuhyo majira ya saa kumi na mbili jioni timu ya JKT Tanzania inayonolewa na kocha Ahmad Ally itakuwa mwenyeji wa Azam iliyo chini ya Florent Ibenge.

JKT Tanzania

JKT inashika nafasi ya nne katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa imekusanya alama nne baada ya kushinda mchezo mmoja dhidi ya Coastal Union na kutoka sare na Mashujaa huku timu ya Azam ikishika nafasi ya tisa baada ya kukusanya alama tatu kwenye mchezo mmoja iliyocheza dhidi ya Mbeya City.

Mchezo wa pili ni kati ya Simba na Namungo utakaopigwa majira ya saa 2:15 usiku ukiwa ni mchezo wa mwisho wa kukamilisha mzunguko wa tatu.

 

Simba SC

 

Simba iliyo chini ya kocha Selemani Matola inashika nafasi ya nane katika msimamo ikikusanya alama tatu katika mchezo wao pekee waliocheza dhidi ya Fountain Gate.

Namungo FC

Namungo ambayo haijapoteza mchezo wowote hadi sasa chini ya kocha Juma Mgunda inakamata nafasi ya tano ikiwa na alama nne baada ya kutoka sare na timu ya Pamba Jiji huku ikiifunga timu ya Tanzania Prisons.