Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) imefanikiwa kufuzu hatua ya Robo Fainali ya michuano ya CHAN2024 inayoendelea katika nchi za Kenya, Tanzania na Uganda na kuwa nchi ya kwanza kujihakikishia kucheza hatua hiyo ya Robo Fainali.
Stars imefika hatua hiyo baada ya jana Agosti 9, kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Madagascar hivyo kujikusanyia alama tisa (9) baada ya kushinda michezo yote mitatu iliyocheza kwenye kundi lake.
Mabao yote ya Stars yalifungwa na Clement Mzize dakika ya pili na ya 21, hii ni kwa mara ya kwanza Clement Mzize anaifungia Timu ya Taifa ya Tanzania kwenye mchezo wa kimashindano.
Na hii ni mara ya kwanza kwa Timu ya Taifa ya Tanzania kufuzu hatua ya Robo Fainali tangu kuanzishwa kwa mashindano haya ya CHAN.
TIKTOKU
Tanzania tmeupga mwing tmuombe mungu atuvushe hatua hii