VITA YA KITAMBI NA GAMONDI NANI KUKAA KILELENI?

Ligi Kuu ya NBC kesho itaendelea Zanzibar kwa mchezo namba 40 utakaozikutanisha timu za Singida Black Star na Yanga utakaochezwa saa 2:30 usiku katika Uwanja wa Amaan, Zanzibar.

Katika mchezo huo timu mbili zinazoongoza msimamo wa Ligi Kuu ya NBC zitakutana, Singida Black Star iliyocheza michezo nane ikiongoza msimamo kwa kuwa na alama 22, ikifunga mabao matatu na kuruhusu nyavu zao ‘kutikiswa’ mara tatu huku ikiwa imeshinda mechi saba na kupata  sare moja.

Kwa upande wa Yanga inayoshikilia nafasi ya pili katika msimamo huo imecheza michezo saba imeshinda mechi zote kwa kufunga mabao 12 na kuvuna alama zote 21 huku ikiwa haijaruhusu nyavu zao ‘kutikiswa’ na wapinzani wao.

Ikumbukwe kuwa utakuwa ni mchezo huo utaamua nani kuwa kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu kati ya Singida ikiongozwa na kocha wake Dennis Kitambi ama Yanga chini ya Miguel Gamondi.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *