YANGA MGUU MMOJA NDANI ROBO FAINALI LIGI YA MABINGWA AFRIKA.

BINGWA mtetezi wa Ligi Kuu ya NBC timu ya Yanga imefanikiwa kupata ushindi wa bao moja ugenini dhidi ya AL Hilal na kujiweka kwenye mazingira mazuri ya kufuzu hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Stephane Aziz Ki ndiye aliyepeleka furaha kwa ‘Wananchi’ baada ya kuipatia bao dakika ya saba kwa shuti kali la nje ya boksi na kuifanya Yanga kukusanya alama zote tatu kutoka nchini Mauritania na kurudi nazo nchini Tanzania.

Yanga inayoshika nafasi ya tatu inahitaji matokeo ya ushindi dhidi ya MC Algers inayoshikilia nafasi ya pili ikiizidi Yanga alama moja ili kujihakikishia nafasi ya kufuzu hatua ya robo fainali ya michuano hiyo.

Yanga inasaka hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa mara ya pili mfululizo baada ya kufanya hivyo msimu uliopita ambapo iliondolewa kwenye hatua ya robo fainali na timu ya Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini.

One comment

Join the Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *