TIMU ya Young Africans imeanza vema kampeni ya kutetea ubingwa wake baada ya kuifunga Namungo kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliochezwa uwanja wa Majaliwa, Ruangwa jana.
Mchezo ulianza kwa kasi kubwa huku Young Africans wakionyesha kuzitaka alama tatu na walifanikiwa kutawala mchezo huo ambapo mpaka kipindi cha kwanza kinatamatika hakuna ambaye alifanikiwa kuingia katika lango la mwenzake .
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi kubwa timu zote zikisaka bao na dakika ya 68 Chadrack Boka wa Young Africans alianza kufungua ukurasa wa mabao huku Max Nzengeli akifunga bao la pili dakika ya 71 ya mchezo huo.
Namungo ilipata bao la kufutia machozi dakika ya 75 na kuweza kumuharibia kipa wa Young Africans Djigui Diarra hati safi yake ya kwanza kwa msimu wa 2026/2027.