Timu ya Ihefu imefanikiwa kushinda mchezo katika uwanja wake wa nyumbani wa Highland Estates dhidi ya Geita Gold ikiwa ni baada ya kupita takribani miezi mitatu tangu ilipoifunga Azam bao 1-0.
Geita imepoteza mchezo wa tatu mfululizo na kuruhusu mabao saba katika michezo hiyo huku ikisalia na alama 37 katika nafasi ya sita.
Ukiwa ni ushindi wa tano katika michezo tisa iliyopita kwa Ihefu unaifanya timu hiyo kufikisha alama 36 na kujihakikishia nafasi ya kushiriki Ligi Kuu msimu ujao.
Mabao ya Bernard Morison (2) na Salum Abubakar yameifanya timu ya Yanga kutoka nyuma na kuilazimisha sare ya mabao matatu Mbeya City kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya.
Mchezo huo ulishuhudia wachezaji Jesus Moloko wa Yanga na Hassan Nassor wa Mbeya City wakishindwa kumaliza mchezo baada ya kuoneshwa kadi nyekundu huku Moloko akitarajiwa kukosa mchezo wa fainali ya kombe la shirikisho utakaochezwa Tanga Juni 12 kwenye uwanja wa Mkwakwani.