PRISONS MAMBO SAFI, MTIBWA IKIILIZA KAGERA

TIMU ya Tanzania Prisons ya Mbeya imejihakikishia nafasi ya kucheza ligi kuu ya NBC msimu ujao baada ya kuifunga KMC ya Dar bao 1-0.

KMC iliyokua na kumbukumbu nzuri ya kushinda mchezo uliopita dhidi ya Singida BS imepoteza kwa bao la mapema kipindi cha kwanza lililofungwa na Edwin Balua.

Prisons imefikisha alama 37 ambazo endapo ikipoteza mchezo wa mwisho haziwezi kufikiwa na timu zilizopo nafasi ya kucheza hatua ya mtoano.

Mabao ya Vitalis Mayanga, Omary Buzungu na bao la kujifunga la Abdallah Mfuko yameongeza matumaini kwa timu ya Mtibwa kuendelea kusalia Ligi Kuu baada ya kuifunga Kagera Sugar mabao 3-0.

Mtibwa imefikisha alama 32 ikihitaji matokeo ya ushindi katika mchezo wa mwisho dhidi ya Geita Gold kujihakikishia nafasi ya kucheza Ligi Kuu msimu ujao.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *