MCHEZO wa watani wa Jadi ‘Kariakoo Derby’ ndani ya Ligi Kuu ya NBC unachezwa leo saa 11:00 jioni kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa.
Mchezo huu ndio ni mkubwa zaidi Tanzania na Afrika mashariki na miongoni mwa ‘Derby’ kubwa zaidi barani Afrika.
Yanga inaingia kwenye mchezo huu ikiwa na kumbukumbu ya ushindi wa mabao 5-1 kwenye mchezo uliopita.
Mwamuzi wa kati kwenye mchezo huu ni Ahmed Arajiga kutoka Manyara, mwamuzi msaidizi namba moja ni Mohamed Mkono kutoka Tanga, mwamuzi msaidizi namba mbili ni Kassim Mpanga kutoka Dar es salaam na mwamuzi wa akiba ni Tatu Malogo kutoka Tanga.