LIGI Kuu ya NBC imeendelea Aprili 20 kwa mchezo wa ‘Kariakoo Derby’ uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa na kumalizika kwa Yanga kuibuka washindi kwa mabao 2-1 dhidi ya Simba.
Yanga imeshinda michezo yote ya Ligi Kuu ya NBC iliyokutana na mtani wake Simba msimu huu wa 2023/24 baada ya mzunguko wa kwanza kupata ushindi mnono wa mabao 5-1 ugenini.
Mabao ya Stephane Aziz Ki aliyefunga kwa mkwaju wa penati na Joseph Guede yametosha kuipa Yanga ushindi huo huku bao pekee la Simba likifungwa na Fred Michael Koublan.
Matokeo hayo yanaifanya Yanga kuwa mbele ya Simba kwa tofauti ya alama 12 huku Simba ikiwa na mchezo mmoja mkononi.
Ligi hiyo itaendelea leo kwa michezo mitatu ambapo mchezo wa mapema timu ya Tabora United itakuwa mwenyeji wa Geita Gold saa 8:00 mchana, saa 10:00 alasiri Singida Fountain Gate itaialika Mashujaa kwenye uwanja wa CCM Kirumba na mchezo wa mwisho utakuwa kati ya Azam FC na Ihefu kwenye uwanja wa Azam Complex.
Kwann stangaze kuwa yanga bingwa