Mtibwa Sugar imeendelea kusalia kileleni mwa msimamo wa Ligi ya Championship ya NBC 2024/2025 baada ya ushindi wa bao moja dhidi ya Songea United Leo kwenye uwanja wa Manungu, Morogoro.
Mtibwa Sugar imefikisha alama 12 kwenye michezo minne iliyocheza hadi sasa ikifunga mabao Saba bila kuruhusu bao lolote.
Michezo mingine miwili ilichezwa leo, Mapema saa 8:00 Mchana Mbeya kwanza iliialika Green Warriors katika uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara na Kumalizika kwa Mbeya Kwanza kuibuka na ushindi wa bao 1-0.
Mchezo mwingine ulizikutanisha Mbuni na Biashara United na kumalizika kwa sare ya bao 1, mchezo huo ulichezwa katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha.