KUFA AU KUPONA ‘KARIAKOO DERBY’ LIGI KUU YA NBC LEO.

LIGI Kuu ya NBC inatarajiwa kuendelea leo kwa mchezo mmoja utakaokutanisha ‘Miamba’ wa Tanzania kwenye soka timu ya Simba itakayokuwa nyumbani kuikaribusha Yanga kwenye uwanja wa Mkapa, Dar saa 11:00 jioni.

Huu ni mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu ya NBC msimu huu kwa timu hizo huku Simba ikiwa na kumbukumbu mbaya ya kupoteza kwenye mchezo uliopita dhidi ya Yanga kwa mabao 2-1.

Simba inaingia kwenye mchezo huu ikiwa imetoka sare ya mabao mawili kwenye mchezo uliopita wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Coastal Union ya Tanga.

Timu ya Yanga itaingia kucheza ugenini leo ikiwa na kumbukumbu nzuri ya kuahinda mchezo uliopita wa Ligi Kuu ya NBC kwa mabao 4-0 dhidi ya timu ya Pamba.

Yanga haijapoteza mchezo wowote wala kuruhusu bao kwenye Ligi Kuu ya NBC msimu huu hadi sasa huku ikiwa na rekodi nzuri ya kushinda michezo yote iliyokutana na Simba msimu uliopita.

One comment

Join the Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *