MWALIMU HASHIKIKI LIGI KUU YA NBC

KINARA wa mabao ndani ya Ligi Kuu ya NBC Selemani Mwalimu wa timu ya Fountain Gate amendelea kuwa mwiba kwa mabeki wa timu pinzani baada ya jana kufunga na kuisaidia timu yake kushinda mchezo wa tano msimu huu.

Fountain iliifunga KMC ya Dar mabao 3-1 kwenye uwanja wa Tanzanite Kwaraa mkoani manyara huku mchezo huo ukimalizika kwa nyota wa KMC Ibrahim Elias kuonyeshwa kadi nyekundu ikiwa ni dakika tisa baada ya kuingia uwanjani.

Mwalimu amefikisha jumla ya mabao sita ndani ya michezo nane aliyocheza huku pia akitoa pasi moja iliyozaa bao kwa Edgar William hapo jana.

Fountain ndio timu iliyofunga mabao mengi hadi sasa ikifikisha mabao 17 na kufuatiwa na Simba yenye mabao 12.

Mchezo mwingine ulichezwa uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma na kushuhudia timu ya Mashujaa ikiifunga KenGold mabao 3-0 na kukwea hadi nafasi ya sita baada ya kufikisha alama 12.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *