YANGA YAENDELEZA UBABE LIGI KUU YA NBC.

Timu ya Yanga imeendeleza ubabe inapocheza dhidi ya Simba baada ya kushinda kwa bao moja kwenye mchezo uliozikutanisha timu hizo kwenye uwanja wa Mkapa, Dar.

Bao la Yanga limepatikana baada ya mchezaji Kelvin Kijili kushindwa kuokoa mpira na kujifunga hivyo kufanya Yanga kushinda mchezo wa tano mfululizo msimu huu.

Hadi sasa Yanga ndio timu pekee ambayo haijaruhusu bao huku ikifunga mabao tisa na kuwa timu kinara wa wastani mzuri wa mabao sawa na timu ya Simba.

Kwa Matokeo hayo Yanga inapanda hadi nafasi ya pili ya msimamo ikikusanya jumla ya alama 15 nyuma ya kinara Singida Black Stars yenye alama 16 baada ya michezo sita.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *