LIGI Kuu ya NBC inaendelea leo kwa michezo miwili ambapo timu ya Prisons inaikaribisha Simba kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya mchezo wa mapema saa 10:00 alasiri.
Prisons inakuwa mwenyeji wa Simba huku ikiwa na kumbukumbu mbaya ya kupoteza mchezo uliopoita dhidi ya Azam kwenye uwanja wa nyumbani kwa mabao 0-2.
Simba inakwenda ugenini ikiwa ni baada ya kupoteza mchezo uliopita kwenye uwanja wa nyumbani dhidi ya Yanga kwa bao moja.
Mchezo wa mwisho utachezwa uwanja wa Azam Complex, Dar kati ya Yanga itakayoikaribisha JKT Tanzania saa 1:00 usiku.
JKT iliyoshinda mchezo uliopita dhidi ya Tabora United kwa mabao 4-2 inakutana na Yanga ambayo haijapoteza mchezo wowote wala kuruhusu bao hadi sasa kwenye msimu huu wa Ligi Kuu ya NBC.