MSHAMBULIAJI wa Yanga Jean Baleke ameibeba timu yake baada ya kufunga bao na kuiwezesha timu hiyo kupata pointi 3 muhimu kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Coastal Union uliochezwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha jana.
Ilimchukua dakika 25 Baleke kuipa timu yake bao katika mchezo ulioonekana mgumu kwa timu zote ambapo zilikuwa zikishambuliana kwa nguvu kabla ya kona kupigwa kuelekea lango la Coastal na kumfanya Baleke kuweza kufunga mpira huo .
Aidha mchezo huo ulikuwa wa kwanza kwa Kocha Juma Mwambusi aliyetangazwa hivi karibuni kama Kocha Mkuu wa Coastal Union ambaye baada ya mchezo huo alisema kuwa amepoteza mchezo kwa mpinzani mgumu anarudi kukaa na timu yake kujitathimini wapi walikosea ili waweze kujirekebisha.
Kwa upande wa Kocha wa Yanga Miguel Gamondi alisema kuwa Ligi Kuu ya NBC msimu huu imekuwa ngumu zaidi kupata matokeo ya kufunga mabao mengi kwani timu zote zinajiandaa vizuri na ikumbukwe kuwa Ligi Kuu ya NBC ni ligi ya 6 kwa ubora barani Afrika.