LIGI KUU NBC YAZIDI KUSHIKA KASI

LIGI Kuu ya NBC inazidi kushika kasi ikiwa ni mzunguko wa 9 wa ligi hiyo ambayo ni Ligi ya 6 kwa ubora barani Afrika na ya kwanza kwa ubora katika ukanda wa CECAFA na pili kwa ukanda wa nchi za kusini mwa Afrika ikiwa nyuma ya Ligi Kuu ya Afrika Kusini.

Ubora wa Ligi Kuu ya NBC umeletwa na ushindani wa klabu 16 zinazoshiriki Ligi hiyo ambazo kila mmoja amekuwa akicheza kwa malengo ya kuleta ushindani huku kila timu ikitaka kuondoka na pointi 3 kwa kila mchezo husika.

Mpaka sasa timu hizo 16 za Ligi Kuu ya NBC zimeweza kufanikiwa kufunga mabao 133 ikiwa ni katika michezo 68 iliyochezwa katika ligi hiyo.

Fountain Gate ndio kinara wa kufunga mabao wakiwa wamefanikiwa kufunga mabao 17 na kuruhusu mabao 15 huku Simba wakiwa na mabao 16 wakiruhusu nyavu zao kutikiswa mara tatu, timu ya tatu ni Singida Black Stars wakiwa na bao 13 wakiruhusu mabao matatu na Yanga wamefunga mabao 12 sawa na Azam huku yanga wakiwa hawajaruhusu bao lolote na Azam wakiwa wameruhusu mabao matatu.

Timu zenye mabao machache ni KenGold iliyofungwa mabao matano na kufungwa 17, Pamba jiji imefunga matatu na kuruhusu 11, Kagera Sugar imefunga manne na kufungwa tisa huku Namungo ikifunga manne na kufungwa 11.

Ligi Kuu ya NBC itaendelea leo jumatatu kwa michezo miwili ambapo mchezo wa kwanza utachezwa saa 10 alasiri kati ya Fountain Gate na Mashujaa katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Manyara na Saa 1:00 usiku Namungo watawakaribisha Pamba Jiji katika Uwanja wa Majaliwa Ruangwa.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *