Ligi Kuu ya NBC imeendelea na kushuhudia michezo miwili ikichezwa katika viwanja vya Tanzanite Kwaraa mkoani Manyara na Majaliwa mkoani Lindi.
Mchezo wa kwanza uliochezwa majira ya jioni timu ya Fountain Gate iliikaribisha timu ya Mashujaa na kushuhudia sare ya mabao 2-2.
Mabao ya Fountain Gate yalifungwa na Nicholas Gyan na Salum Kihimbwa huku magoli ya Mashujaa yakifungwa na Seif Karihe na Hassan Ali.
Mchezo wa pili uliochezwa Uwanja wa Majaliwa Lindi timu ya Namungo waliwakaribisha Pamba Jiji ya Mwanza katika mchezo ambao wenyeji Namungo walifanikiwa kubaki na alama tatu muhimu za mchezo huo baada ya mchezaji wao Ibrahim Abdallah kufunga goli pekee dakika ya 14 ya mchezo huo.
Ligi ya NBC leo itaendelea kwa michezo miwili ambapo KenGold watawakaribisha Dodoma Jiji katika Uwanja wa Sokoine Mbeya na Coastal Union watawakaribisha Kagera Sugar Uwanja wa Sheikhe Amri Abeid jijini Arusha huku michezo yote ikitarajiwa kuanza saa 10:00 alasiri.