BAADA ya kupoteza dhidi ya Azam, leo timu ya Yanga inashuka uwanjani kuikaribisha Tabora United ya Tabora saa 12:00 jioni kwenye uwanja wa Azam Complex, Dar.
Yanga iliyopoteza mchezo uliopita nyumbani leo itakuwa tena mwenyeji wa Tabora iliyopata ushindi kwenye mchezo wake uliopita dhidi ya Mashujaa kwa bao 1-0.
Yanga itajaribu kupata ushindi leo ili kurejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya NBC baada ya kupoteza nafasi hiyo inayoshikiliwa na Simba kwa sasa baada ya kushinda mchezo wa jana dhidi ya KMC.
Hadi sasa Yanga imefungwa mchezo mmoja na bao moja pekee ikiwa timu ya pili kwa wastani mzuri wa mabao (12) nyuma ya Simba yenye (18).