Kiungo wa Simba Jean Ahoua amekuwa tishio katika Ligi Kuu ya NBC baada ya kuchangia mabao 9 kati ya 21 ambayo timu yake ya Simba imefunga katika mizunguko 10 iliyocheza.
Ahoua ambaye amesajiliwa na Simba mwanzoni mwa msimu huu amefanikiwa kufunga mabao matano katika Ligi Kuu na kuhusika katika pasi nne zilizozaa mabao.
Mchezaji huyo pia amefanikiwa kuchukua tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Agosti na pia amechukua tuzo mbili za mchezaji bora wa mechi kati ya Simba na Fountain Gate baada ya kufunga bao moja na kutoa pasi ya mwisho moja na mchezo kati ya Simba na KMC alipofunga mabao mawili hivyo kuchangia ushindi wa mabao manne ilioupata timu yake.
Ligi Kuu ya NBC inazidi kushika kasi ambapo mpaka sasa timu nyingi zimekuwa zikileta ushindani na upinzani mgumu jambo linalodhihirisha ubora wa Ligi hii