JKT, PAMBA HAKUNA MBABE LIGI KUU YA NBC

LIGI Kuu ya NBC imeendelea kwa mzunguko wa 14 kuchezwa michezo miwili iliyopigwa mkoani Dar es Salaam na Kagera.

Timu ya JKT Tanzania ilikuwa mwenyeji wa Pamba Jiji ya Mwanza katika uwanja wa Isamuhyo, Dar es Salaam saa kumi alasiri na kumalizika kwa suluhu.

Katika mchezo huo golikipa wa Pamba Jiji Yona Amos alitangazwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo baada ya kuokoa mashambulizi mengi yaliyolenga lango lake.

Mchezo mwingine ulichezwa uwanja wa Kaitaba, Kagera na kushuhudia Kagera Sugar ikiialika Namungo katika mchezo ulioisha kwa sare ya 1-1.

Dakika ya 64 ya mchezo huo Kagera Sugar walijibu mapigo kupitia mchezaji wao Peter Lwasa aliyesawazisha na kufanya mchezo huo kumalizika kwa sare huku Erick Mwijage wa Kagera akitangazwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.

Ligi Kuu itaendelea leo kwa michezo miwili Singida Black Stars watawakaribisha Dodoma Jiji saa nane mchana na KMC watawakaribisha Mashujaa saa kumi jioni kwenye uwanja wa KMC, Dar.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *