TIMU ya Simba inayoshiriki Ligi Kuu ya NBC imefanikiwa kufuzu hatua ya robo fainali ya kombe la Shirikisho Afrika baada ya kupata sare ya bao 1-1 ugenini dhidi ya timu ya Bravos de Marquiz ya Angola.
Leonel Ateba ndiye alikuwa shujaa wa Simba baada ya kusawazisha bao dakika ya 69 lililoifanya timu yake kufikisha alama 10 ambazo haziwezi kufikiwa na Bravos waliopoteza mchezo wa raundi ya kwanza dhidi ya Simba nchini Tanzania huku timu ya Sfaxien ikiburuza mkia bila alama .
Simba imefunga bao kwenye kila mchezo wa kombe la shirikisho msimu huu huku ikipoteza mchezo mmoja pekee dhidi ya CS Constantine.
Vinara hao wa Ligi Kuu ya NBC wanatarajiwa kucheza mchezo wa mwisho dhidi ya CS Constantine kwenye uwanja wa Mkapa, Dar na endapo watafanikiwa kushinda mchezo huo watafuzu hatua ya robo fainali kama vinara kwenye kundi lao.