SILLAH AWALIZA ‘WATOTO WA MJINI’ LIGI KUU NBC

MCHEZAJI wa Azam Gibril Sillah amepeleka kilio kwa KMC ‘Watoto wa mjini’ baada ya kufunga mabao mawili kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliochezwa uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.

Azam ilizitafuta kwa nguvu alama tatu ikicheza kwa kasi huku KMC  ikicheza kwa tahadhari kubwa na kujilinda ingawa Ilimchukua dakika 26 mchezaji wa Azam Gibril Sillah kufungua akaunti ya mabao na hadi mapumziko Azam ilienda kifua mbele ikiongoza kwa bao 1-0.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku KMC ikionekana kutaka kusawazisha kwa kuwashambulia Azam ambao muda wote waliziba njia na mipango ya KMC na dakika ya 65 Sillah alirejea tena ‘kambani’  na kufanya ubao kusomeka 2-0.

Mpaka mchezo huo unatamatika Azam ilifanikiwa kubakisha alama tatu muhimu za mchezo huo wakiendelea kuwa nafasi ya tatu na alama 39 katika msimamo huo.

Matokeo hayo yanaifanya Azam kupata ushindi kwenye michezo yote miwili iliyocheza dhidi ya KMC msimu huu baada ya mzunguko wa kwanza kuifunga mabao 4-0 kwenye uwanja wa KMC Complex, Dar.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *