TIMU ya Dodoma Jiji imepoteza mchezo wake wa kwanza wa Ligi Kuu ya NBC baada ya kurejea kutoka kwenye mapumziko mafupi kwa bao moja kutoka kwa Pamba Jiji ya mkoani Mwanza.
Mchezo huo uliokutanisha timu zilizopo chini ya manispaa za jiji ulipigwa kwenye uwanja wa Jamhuri, Dodoma na kushuhudia bao lililofungwa kipindi cha kwanza na Mathew Tigisi likiizamisha Dodoma nyumbani.
Huu ni mchezo wa tatu kwa timu ya Pamba kushinda kwenye Ligi Kuu ya NBC msimu huu huku ikishinda miwili ugenini na mmoja pekee ikishinda kwenye uwanja wake wa nyumbani.
Dodoma imepoteza mchezo wa nane msimu huu idadi sawa na timu ya Pamba jiji huku Dodoma ikisalia nafasi ya tisa na alama 19 nne zaidi ya timu ya Pamba iliyofikisha alama 15 na kushika nafasi ya 14.