KEN GOLD ‘HALI TETE’ LIGI KUU YA NBC.

TIMU ya KenGold kutoka mkoani Mbeya imeendelea kujiweka kwenye wakati mgumu wa kushiriki Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2025/26 baada ya kupoteza mchezo wa 14 wa ligi hiyo msimu huu dhidi ya Azam kwa mabao 2-0 kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya.

KenGold inayoshika nafasi ya mwisho kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC imepoteza mchezo wa 14 msimu huu na kuwa timu iliyofungwa michezo mingi sawa na timu ya Prisons ya Mkoani Mbeya pia.

Mabao ya Gibril Sillah na Nassor Saadun yalitosha kuipa Azam alama tatu muhimu huku golikipa Zuber Foba akimaliza mchezo bila kuruhusu bao na kufikisha idadi ya hati safi ‘Cleansheet’ ya tano msimu huu.

Azam imeendelea kujiweka katika nafasi nzuri ya kuwania ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC msimu huu ikifikisha jumla ya alama 51 ikizidiwa alama sita pekee na Simba inayoshika nafasi ya pili na alama 10 nyuma ya kinara Yanga.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *