COASTAL UNION YATAMBA MKWAKWANI.

Ligi Kuu ya NBC ilitimua vumbi tena kwenye uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga majira saa moja jioni ambapo ulizikutanisha timu ya Coastal union na Kengold na Coastal kushinda 2-1.

Timu zote zilikuwa na shauku ya kupata alama tatu muhimu na hasa Kengold ambayo ipo nafasi ya mwisho katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC na ushindi pekee ungeweka  matumaini yao ya kusalia ligi kuu.

Dakika ya 20 Bakari Msimu wa Coastal Union aliipatia bao la kwanza timu yake na kuamsha mashabiki kwa shangwe na dakika ya 37 mchezaji Amara Bagayoko alipigilia msumari wa pili na kuzima matumaini ya KenGold kusalia ligi kuu.

Dakika ya 39 zikiwa zimesalia dakika 6 kipindi cha kwanza kutamatika Kengold  ilipata bao pekee lililofungwa na Sadalah Lipangile hivyo mchezo kumalizika 2-1.

Ushindi huo umeiweka Coastal union nafasi ya 8 na alama 31 huku Kengold ikiwa nafasi ya 16 ambayo ni ya mwisho ikiwa na alama 16 na kushuka daraja rasmi.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *