KENGOLD YAAGA RASMI LIGI KUU YA NBC.

TIMU ya KenGold imekuwa timu ya kwanza kuaga Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2024/25 na kushuka daraja baada ya kupoteza jana kwa mabao 2-1 dhidi ya Coastal Union ya Tanga kwenye uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

KenGold iliyokuwa bingwa wa Ligi ya Championship ya NBC msimu wa 2023/24 na kufanikiwa kupanda ligi kuu imedumu kwa msimu mmoja pekee na kurejea tena kwenye ligi ya Championship.

Hadi sasa mabingwa hao waliopita wa Championship wameshinda michezo mitatu pekee ya Ligi Kuu ya NBC wakifungwa 17, huku wakitoka sare michezo saba na kukusanya alama 16 pekee huku ikisalia michezo mitatu kukamilika kwa msimu.

KenGold hadi sasa imeruhusu mabao 50 na kufunga 22 huku ikiwa timu ya pili kuruhusu mabao mengi nyuma ya Fountain Gate ya Manyara iliyofungwa mabao 51 hadi sasa.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *