PAZIA la Ligi ya Championship ya NBC linafungwa leo Mei 11 kwa michezo nane kupigwa kwenye viwanja nane tofauti kuanzia saa 10:00 alasiri.
Michezo ya Leo itamtambulisha bingwa wa Ligi ya Championship ya NBC Kati ya Mtibwa Sugar au Mbeya City pia kujua ni timu gani itaungana na Biashara United kushuka daraja.
Mtibwa ili kuwa bingwa inahitaji alama moja pekee ili kufikisha alama 69 ambazo haziwezi kufikiwa na Mbeya City na endapo Mbeya City itapata matokeo yoyote tofauti na ushindi Mtibwa itakuwa bingwa.
Kwa upande wa Mbeya City inahitaji kushinda ili kufikisha alama 68 na endapo Mtibwa ikipoteza mchezo wa leo timu hizo zitalingana alama na Mbeya City atakuwa bingwa kwa tofauti ya mabao.
Vita nyengine ni ya kushuka daraja ambapo klabu za African Sports, Cosmopolitan na Transit Camp zipo kwenye hatari ya kushuka na kuungana na Biashara United.
African Sports ina alama 19 wakati Cosmopolitan ina alama 20 na Transit Camp ikiwa na alama 21, michezo ya mwisho hii Leo itatoa hatma ya timu hizo msimu huu