CARGO, KAJUNA ZATAMBA NYUMBANI MTOANO FIRST LEAGUE.

Michezo ya mtoano (PlayOff) kubaki au kupanda ligi ya First League imechezwa Jana Mei 8 ikishuhudiwa timu zilizokuwa nyumbani Cargo ya Dar na Kajuna ya Kigoma zikiibuka na ushindi.

Mchezo wa kwanza katika uwanja wa TFF Center – Kigamboni uliishuhudia Cargo ikiibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Tunduru Korosho.

Mchezo wa pili mkoani Kigoma uliishuhudia Kajuna ikiifunga Copco ya Mwanza kwa mabao 2-0 kwenye uwanja wa Lake Tanganyika.

Michezo ya marudiano itapigwa Mei 12 ambapo Tunduru Korosho itaialika Cargo kwenye uwanja wa Majimaji mkoani Ruvuma huku Copco ikiialika Kajuna kwenye uwanja wa Nyamagana mkoani Mwanza.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *