MTIBWA SUGAR MABINGWA LIGI YA CHAMPIONSHIP YA NBC 2024/2025.

TIMU ya Mtibwa Sugar ya mkoani Morogoro imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi ya Championship ya NBC msimu wa 2024/2025.

Mtibwa Sugar kwenye mchezo wake wa mwisho hii Leo dhidi ya Kiluvya iliyochezwa kwenye uwanja wa Manungu Complex imefanikiwa kuibuka na kushinda wa mabao 2-0 myaliyofungwa na Raizin Hafidh dakika ya 36 na 46 ya mchezo huo.

Baada ya ushindi huo Mtibwa Sugar inafikisha alama 71 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote inayoshiriki Ligi ya Championship ya NBC.

Mtibwa Sugar ambayo ilishuka daraja kutoka Ligi Kuu ya NBC msimu uliopita imefanikiwa kufunga mabao 58 huku ikifungwa mabao 18 hivyo kujihakikisha nafasi ya kushiriki Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2025/2026.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *