SIMBA ‘YAIBAMIZA’ KMC LIGI KUU NBC

LIGI Kuu ya NBC imeendelea leo kwa mchezo mmoja uliochezwa uwanja wa KMC Complex, mkoani Dar es Salaam kati ya KMC ikiikaribisha timu ya Simba na kushuhudia ‘Mnyama’ akishinda 1-2 ugenini.

Mchezo huo ulianza majira ya saa kumi alasiri kwa timu zote kuwa na ari ya kuzitaka alama tatu muhimu KMC ikitaka kujihakikishia nafasi ya kusalia Ligi Kuu ya NBC msimu ujao huku Simba ikijiimarisha kwenye mbio za ubingwa.

Dakika nane ziliitosha timu ya KMC kufungua ukurasa wa mabao kupitia kwa Rashid Chambo kabla ya timu ya Simba kusawazika kupitia mshambuliaji wake Steven Mukwala dakika ya 15 ya mchezo na dakika 46 aliongeza bao la pili hivyo mchezo kumalizika kwa 1-2.

Simba imefikisha alama 69 ikiwa nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikifunga mabao 62 na kuruhusu mabao 11 katika michezo 26 ambayo timu hiyo imecheza huku KMC ikiwa nafasi ya 11 na alama 30 ikifunga mabao 23 na kuruhusu mabao 41 katika michezo 27 ambayo timu hiyo imeshacheza.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *