CAMARA MKALI WA ‘HATI SAFI’ LIGI KUU YA NBC.

GOLIKIPA wa timu ya Simba, Moussa Camara ameendeleza moto wake wa kuongoza kwa kuwa na hati safi nyingi kuliko magolikipa wengine wa timu za Ligi Kuu ya NBC akiwa hajaruhusu bao kwenye michezo 16 akiwa kwenye msimu wa kwanza ndani ya Simba.

Camara mpaka sasa amecheza michezo 24 sawa na dakika 2160 huku timu yake ya Simba ikiwa nafasi ya pili kwenye msimamo nyuma ya Young Africans inayoshikilia usukani.

Golikipa wa Young Africans,Djigui Diarra anafuatia akiwa amecheza dakika 1819 katika michezo 20 ya Ligi Kuu ya NBC amefanikiwa kukusanya hati safi 14.

Patrick Munthali wa timu ya Mashujaa kutoka Kigoma anashika nafasi ya tatu akiwa amefanikiwa kukusanya hati safi 12 huku Mohamed Mustapha wa timu ya Azam akishika nafasi ya nne na hati safi 10.

Nafasi ya tano inashikiliwa na Yona Amos wa Pamba Jiji aliyefanikiwa kukusanya hati safi tisa huku Yakoub Suleiman wa JKT Tanzania amekusanya hati nane akishika nafasi ya sita.

Metacha Mnata wa Singida Black Stars na Ngaleka Katembua wa Dodoma Jiji wanafunga orodha wakifanikiwa kukusanya hati safi saba kila mmoja.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *