STAND UNITED, FOUNTAIN GATE NI VITA YA KUCHEZA LIGI KUU YA NBC.

 

HATUA ya mtoano wa nani kusalia ama kupanda Ligi Kuu ya NBC inaendelea kesho kwa mchezo mmoja kati ya Stand United ya mkoani Shinyanga itakayokuwa mwenyeji wa timu ya Fountain Gate kwenye uwanja wa Kambarage mkoani Shinyanga.

Mchezo huo utakaopigwa saa kumi alasiri utakuwa muhimu kwa timu zote ili kujihakikishia kucheza kwenye ligi namba nne kwa ubora barani Afrika.

Stand United ambao msimu wa 2024/2025 imecheza Ligi ya championship ya NBC inapaswa kupata ushindi wa matokeo ya jumla ya michezo ya nyumbani na ugenini ili kupanda Daraja huku timu ya Fountain Gate nayo ikipaswa kufanya hivyo ili kuhakikisha inabaki Ligi Kuu ya NBC msimu ujao.

Stand imepata nafasi ya kucheza hatua ya mtoano baada ya kuitoa timu ya Geita Gold kwa matokeo ya jumla huku Fountain ikicheza baada ya kupoteza kwenye matokeo ya jumla dhidi ya Tanzania Prisons.

Tatu Malogo kutoka Tanga ndiye mwamuzi atakaesimamia mchezo huo wa kwanza akisaidiwa na Hamdan Said kutoka Mtwara, Zawadi Yusuph kutoka Dar es Salaam na Shija Shurugwai kutoka mkoani Shinyanga.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *