TIMU ya Tanzania Prisons imefanikiwa kusalia Ligi Kuu ya NBC baada ya kuifunga timu ya Fountain Gate 3-1 katika mchezo uliochezwa uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya.
Ilimchukua dakika saba mchezaji wa Tanzania Prisons,Beno Ngasa kufungua ukurasa wa mabao huku mchezaji wa Fountain Gate Laurian Makame akisawazisha dakika ya 27 kabla ya Ezekiel Mwashilindi kuiongezea Prisons bao dakika ya 45 hivyo maafande hao Kwenda mapumziko wakiongoza 2-1.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo dakika ya 47 ya mchezo huo mchezaji wa Prisons Oscar Mwajanga aliongeza bao la tatu kwa timu hiyo na matokeo yakisalia hivyo mpaka mwisho wa mchezo .
Tanzania Prisons wamesalia Ligi Kuu ya NBC kwa uwiano wa mabao 4-2 katika michezo yote miwili ambayo timu hiyo na Fountain Gate zimecheza.
Hongera prison