OKELLO, BARKER WANG’ARA TUZO MEI.

KIUNGO mshambuliaji  wa Young Africans, Allan Okello, amechaguliwa kuwa mchezaji Bora wa mwezi Mei wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa mwaka 2025/26, huku Steve Barker wa Simba  akichaguliwa Kocha Bora wa ligi hiyo kwa mwezi huo.

Mchezaji wa Young Africans, Allan Okello.

Okello alionyesha kiwango kizuri chenye mwendelezo kwa mwezi huo ikiwa ni pamoja na kufunga mabao tisa na kuhusika na lingine moja kwa kutoa pasi ya usaidizi  katika dakika 509 za michezo sita, ambayo Young Africans ilicheza nakuisaidia kubaki kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

Mchezaji huyo aliwashinda viungo Clatous Chama wa Simba na Feisal Salum wa Azam alioingia nao fainali katika mchakato wa Tuzo za Mwezi uliofanywa na Kamati ya Tuzo za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Kocha Mkuu wa Simba Steve Barker.

Kwa upande wa Barker aliyeingia fainali na Florent Ibenge wa Azam na Fred Minziro wa Fountain Gate, aliiongoza timu yake kushinda michezo mitanoi liyocheza na kutoka sare mmoja na kuendelea kubaki nafasi ya pili kwenyemsimamo wa ligi.

Wakati huohuo Meneja wa Uwanja wa Airtel Singida, Omar Malule amechaguliwa kuwa Meneja Bora wa Uwanja kwa mwezi Mei kutokana na kufanya vizuri katika menejimenti ya matukio ya michezo pamoja na masuala yanayohusu miundombinu uwanjani.

Katika hatua nyingine Salum Mlemwa wa Gunners amechaguliwa Mchezaji Bora waMwezi Mei wa Ligi ya NBC Championship 2025/26, huku Henry Mkanwa pia waGunners akichaguliwa Kocha Bora wa mwezi huo.

Mlemwa aliyeingia fainali na Richardson Ng’ondya wa Geita Gold na Maulid Shaaban wa Geita Gold, alionyesha kiwango chenye mwendelezo ikiwa ni pamoja na kufunga mabao manne kwa dakika  357  za michezo mitano aliyocheza.

Kwa upande wa Mkanwa aliyeingia fainali na Twaha Beimbaya wa B19 na Mbwana Makata wa Polisi Tanzania, aliiongoza timu yake kushinda michezo yote minne iliyocheza na kupaa kutoka nafasi ya 11 hadi ya saba kwenye msimamo wa Ligi yaChampionship ya NBC.

Pia Kamati ya Tuzo iliteua mabao matatu bora yatakayopigiwa kura na mashabikiili kupata bao bora la mwezi. Mabao hayo ni la Paul Peter (JKT Tanzania vs Fountain Gate dakika ya 85), Clatous Chama (Simba SC vs Young Africans, dakika ya 9) na Christopher Tibandeke (TRA United vs Mtibwa Sugar dakika ya 8).

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *