IMESALIA Siku moja pekee kwa miamba ya soka nchini Tanzania Simba na Yanga kukutana katika mchezo wa duru la pili katika Ligi Kuu ya NBC utakaopigwa majira ya 11:00 jioni kwenye uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam jumapili Aprili 16 .
Fiston Mayele wa Yanga ndiye kinara wa kufunga mabao katika michezo ya Ligi Kuu akifunga 16 huku akifuatiwa na Moses Phiri wa Simba mwenye mabao 10.
Said Ntibazonkiza ndiye mchezaji aliehusika katika mabao mengi kwenye Ligi Kuu ya NBC (19) akifunga mabao 10 na kutoa pasi za mabao tisa huku akifuatiwa na Fiston Mayele wa Yanga aliehusika katika mabao 18 akifunga 16 na kutoa pasi mbili za mabao.
Timu hizo zinakutana Simba ikiwa kinara wa kufunga mabao katika Ligi Kuu NBC ikifunga mabao 60 huku Yanga ikishika nafasi ya pili na mabao 50.