TIMU ya Yanga imefanikiwa kufuzu fainali ya Ngao ya Jamii baada ya kushinda mabao 2-0 dhidi ya Azam katika uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
Azam iliyokuwa imejichimbia nchini Tunisia kwa maandalizi ya msimu mpya imeshindwa kutamba na kuruhusu mabao hayo mawili yaliyofungwa na Stephane Aziz Ki na Clement Mzize walioingia kipindi cha pili.
Matokeo hayo yanaifanya Azam kusubiri timu itakayopoteza nusu fainali ya pili hapo kesho kati ya Simba na Singida Big Stars ili kucheza na kutafuta nafasi ya mshindi wa tatu.
Timu ya Yanga itasubiri mshindi kati ya Simba na Singida ili kucheza fainali itakayopigwa Agosti 13 kwenye uwanja wa Mkwakwani na kujaribu kutetea taji hilo baada ya kulitwaa kwa miaka miwili mfululizo iliyopita.