PAZIA la Ligi ya NBC Championship lilifunguliwa rasmi jana septemba, 9 kwa michezo mitatu kuchezwa.
Ligi hiyo itaendelea tena leo kwa michezo minne kati ya TMA na Stand United kwenye uwanja Sheikh Amri Abeid,Arusha saa 8:00 mchana.
Mchezo wa pili utazikutanisha Ken Gold dhidi ya Transit Camp uwanja wa Sokoine, Mbeya saa 10:00 alasiri.
Mchezo wa tatu ni Kati ya FGA Talents na Ruvu Shooting uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro saa 10:00 alasiri na Mchezo wa mwisho Mbuni atakuwa mwenyeji wa Biashara United kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha saa 10:00 alasiri.