WARATIBU ‘WANOLEWA’ DAR.

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa kushirikiana na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) leo Septemba 9, imeendesha semina ya waratibu wa michezo iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano Benjamin Mkapa Dar es saalam.

Semina hiyo ilikuwa na lengo la kuwaongezea ufanisi katika kusimamia michezo mbalimbali ya kimashindano iliyo chini ya TFF na TPLB.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina hiyo Afisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi Kuu Almasi Kasongo amesema lengo la semina hiyo ni kuongeza ufanisi na uwezo wa waratibu katika usimamizi wa michezo inayoendeshwa chini ya TFF na Bodi ya ligi.

Kasongo amewataka waratibu wa michezo kuwa mabalozi Wazuri wa Bodi ya Ligi na TFF katika usimamizi wa michezo.

“Ligi yetu ni ya 5 kwa ubora na hili limefanikiwa kwa mchango wenu katika kusimamia michezo hii vizuri hivyo niwaombe muendelee kuwa bora zaidi kupitia mafunzo haya” alisema Kasongo.

Miongoni mwa mada zilizowasilishwa ni pamoja na udhamini wa ligi na mipangilio (League sponsorship and branding), taratibu za mchezo (Match Coordination), taratibu za habari siku ya mchezo (Match day media operations) na Kanuni (Regulations).

Semina hiyo imehudhuriwa na waratibu Zaidi ya 30 kutoka mikoa zaidi ya 22 Tanzania Pamoja na watumishi wa Bodi ya Ligi na TFF.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *