PAMBA YAANZA KIBABE NBC CHAMPIONSHIP

LIGI ya NBC Championship imeendelea leo Septemba 11 kwa mchezo mmoja kuchezwa kati ya Pamba Jiji ya Mwanza na Cosmopoilitan ya Dar uliomalizika kwa Cosmo kupoteza kwa mabao 4-0.

Mchezo huo uliopigwa katika uwanja wa Nyamagana mkoani Mwanza umeshuhudiwa Cosmo waliokuwa mabingwa wa First League msimu wa 2022-2023 wakienda mapumziko wakiwa wameruhusu mabao matatu.

“Hii timu ina malengo yake, niliwaambia wachezaji tunahitaji sana kupanda Ligi Kuu ya NBC na endapo tukifungwa sana isiwe zaidi ya mechi mbili na wametekeleza majukumu tumeweza kupata ushindi” amesema kocha mkuu wa Pamba Mbwana Makata.

Kwa ushindi huo Pamba imepanda moja kwa moja kileleni mwa msimamo wa Ligi ya NBC Championship kwa tofauti ya idadi ya mabao juu ya timu za Mbeya City, Pan Africans na FGA Talents walioshinda michezo yao kwanza kama ilivyo kwa Pamba.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *