NBC CHAMPIONSHIP LIVE TV3

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) leo Septemba 13 wameingia mkataba wa miaka mitatu (3) wa haki za matangazo ya televisheni kwa ligi ya NBC Championship na TV3 wenye thamani ya shilingi Milioni 613 kuanzia msimu wa 2023/2024 mpaka 2025/2026.

Akizungumza wakati wa hafla ya makubaliano hayo Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia amesema wanaishukuru TV3 kwa kuamua kuonyesha Ligi ya NBC Championship na kuwahakikishia hawatojutia udhamini wao.

“Niwahakikishie TV3 hamtojuta kuingia mkataba huu na TFF, katika hili tunaenda sambamba kuhakikisha kwamba viwanja vitakavyotumika kwenye NBC Championship viwe na sifa sawa na vile vya Ligi Kuu” alisema Karia.

Naye Msimamizi wa vipindi wa TV3 Emanuel Skawa amesema TV3 wataonesha zaidi ya mechi 170 kati ya mechi 240 za NBC Championship kutokana sababu mbalimbali.

“Mechi hizo zitaonekana kupitia TV3 na TV3 Sports ambayo tutaizindua hivi karibuni na zinapatikana katika kisimbuzi cha StarTimes” alisema Skawa.

TV3 inapatikana ndani ya kisimbuzi cha StarTimes ambacho kinaonekana zaidi ya nchi saba Afrika (Tanzania, Burundi, Rwanda, Kenya, Uganda, Zambia, Msumbiji na Afrika Kusini) hivyo kuweka fursa kwa wachezaji wa Ligi hiyo kuweza kujiuza na kuonekana zaidi.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *