TIMU za Ihefu na Tanzania Prisons zinashuka uwanjani leo kwenye mchezo pekee wa Ligi Kuu ya NBC utakaochezwa kwenye uwanja wa Highland Estates, Mbeya saa 10:00 alasiri.
Ihefu inashuka uwanjani ikiwa haijashinda katika michezo saba iliyopita ikikusanya alama tisa na kushika nafasi ya 14 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.
Tanzania Prisons inaingia uwanjani ikiwa imeshinda mchezo uliopita nyumbani dhidi ya Dodoma Jiji kwa bao 1-0 na kukusanya alama 10 huku ikishika nafasi ya 13 kwenye msimamo.