GEITA YATAMBA, KAGERA IKIBANWA LIGI KUU YA NBC.

TIMU ya Geita Gold ya mkoani Geita imepata ushindi katika uwanja wa nyumbani wa Nyankumbu kwenye Ligi Kuu ya NBC msimu huu baada ya kuifunga JKT Tanzania ya Dar es salaam bao 1-0.

Huu ni ushindi wa pili kwa Geita msimu huu unaowafanya kufikisha alama 10 katika nafasi ya 10 ikipoteza michezo minne na kutoa sare minne.

Kagera imeshindwa kutamba nyumbani dhidi ya KMC baada ya kulazimishwa sare ya bao moja kwenye uwanja wa nyumbani Kaitaba mkoani Kagera.

Bao namba 10 kwa KMC msimu huu lililofungwa na Waziri Junior kwenye mchezo wa leo limeifanya KMC kusalia nafasi ya nne kwenye msimamo ikiwa na alama 16 huku bao la Kagera likifungwa na Deus Bukenya na kuwafanya Kagera kukaa nafasi ya saba ikiwa na alama 13.

Ligi Kuu ya NBC itaendelea tena kesho Novemba 23, Tanzania Prisons ikiikaribisha Coastal union kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya saa 10:00 alasiri huku Namungo ikiwa mwenyeji wa Ihefu kwenye uwanja wa Majaliwa, Lindi saa 1:00 usiku.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *