Ligi ya NBC Championship inaendelea leo kwa Mchezo mmoja kati ya Transit Camp na Ken Gold saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro.
Transit Camp wapo nafasi ya 13 wakiwa na alama 13 baada ya michezo 15 huku Ken Gold wakiwa kileleni mwa msimamo wakiwa na alama 35 baada ya michezo 15.
Ligi hiyo itaendelea tena kesho kwa michezo minne katika mikoa mitatu tofauti.