NBC CHAMPIONSHIP KUPIGWA MIKOA MITATU TOFAUTI LEO.

 

LIGI ya NBC Championship inaendelea leo Januari 6, 2024 kwa michezo minne kuchezwa kwenye mikoa mitatu tofauti.

Michezo ya mapema saa 8:00 mchana itazikutanisha Pan African na Copco katika uwanja wa Mabatini mkoani Pwani, na mchezo mwingine Polisi Tanzania watawaalika Mbeya Kwanza katika uwanja wa Ushirika, Kilimanjaro.

Green Warriors watakuwa wenyeji wa Mbeya City saa 10:00 alasiri katika uwanja wa Mabatini mkoani Pwani, huku Stand United wakicheza na TMA katika uwanja wa Mwadui Complex, Shinyanga.

Ken Gold wapo kileleni mwa msimamo wa Ligi hiyo wakiwa na jumla ya alama 36 baada ya michezo 16, Mbeya kwanza wanashika nafasi ya pili wakiwa na alama 32 baada ya michezo 15 huku nafasi ya tatu ikishikwa na Pamba akiwa na alama 31 baada ya michezo 15.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *