Mwakilishi wa Ligi Kuu ya NBC Simba anahitimisha hatua ya makundi ya kombe la Mapinduzi leo kwa mchezo dhidi ya wababe wa Rwanda APR saa 2:15 usiku kwenye uwanja wa New Amaan Complex.
Simba inaingia katika mchezo huu akiwa kileleni mwa msimamo wa kundi B baada ya kushinda michezo yote miwili ya mwanzo dhidi ya JKU na Singida FG hivyo kua na jumla ya alama sita.
Kwa upande wa APR wamekusanya alama tatu baada ya kushinda mchezo mmoja na kufungwa mchezo mmoja.