MZUNGUKO wa 17 Ligi ya NBC Championship umeanza leo kwa michezo miwili Kupigwa.
Cosmopolitan ikiwa katika uwanja wake wa nyumbani Mabatini mkoani Pwani ikaibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Copco.
Saa 10:00 alasiri Biashara iliwaalika TMA kwenye uwanja wa Karume, Mara na kumalizika kwa Biashara kuibuka na ushindi wa mabao 3-2.
Biashara sasa Imepanda hadi nafasi ya pili ikiwa na alama 36 sawa na Ken Gold wakitofautiana magoli ya kufunga na kufungwa na idadi ya michezo Biashara ikiwa na michezo 17 huku Ken Gold ikiwa na michezo 16.