MICHEZO MITATU NBC CHAMPIONSHIP KUPIGWA LEO.

 

LIGI ya NBC Championship inarejea leo Januari 26 kwa michezo mitatu ya mzunguko wa 19 kuchezwa kwenye mikoa mitatu
tofauti.

Mapema saa 8:00 mchana Copco itawaalika Stand United kwenye uwanja wa Nyamagana mkoani Mwanza, Copco inashika nafasi ya 15 kwenye msimamo ikicheza jumla ya michezo 18 na kupata alama 13 huku Stand United ikishika nafasi ya tisa ikicheza jumla ya michezo 18 ikiwa na alama 22.

Mchezo wa pili utazikutanisha FGA Talents dhidi ya Green Warriors saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro.

Mkoani Arusha Mbuni itakuwa mwenyeji wa Cosmopolitan saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

Mechi zote zitakuwa mubashara kupitia chaneli za TV3 na ST BONGO zinazopatikana kwenye king’amuzi cha Startimes.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *