MBEYA KWANZA YAIBAMIZA BIASHARA NBC CHAMPIONSHIP IKIENDELEA.

 

LIGI ya NBC Championship imeendelea leo Machi 24, 2024 kwa michezo miwili kuchezwa kwenye mikoa ya Mtwara na Morogoro.

Mkoani Mtwara saa 10:00 alasiri Mbeya Kwanza ikaibamiza Biashara United kwa bao 1-0 kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona, bao pekee la Mbeya Kwanza likifungwa na Magata Charles Dakika ya 90+4 ya mchezo.

Kwa Matokeo haya Mbeya Kwanza inapanda hadi nafasi ya nne kwenye msimamo ikifikisha alama 53 sawa na Biashara United ikizidiwa utofauti wa mabao ya kufunga na kufungwa Biashara ikiwa na 29 huku Mbeya Kwanza ikiwa na 17.

Mchezo mwengine ukazikutanisha Transit Camp dhidi ya Cosmopolitan saa 10:00 alasiri kwenye uwanja wa Jamhuri, Morogoro na kumalizika kwa Transit Camp kufungwa 1-2 mbele ya Cosmopolitan.

Mzunguko wa 26 utamatika kesho kwa mchezo Kati ya Green Warriors dhidi ya Pan Africans kwenye uwanja wa Mabatini mkoani Pwani sa 10:00 alasiri.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *