MICHEZO mitatu ya Ligi ya NBC Championship imechezwa leo kwenye viwanja mbalimbali ndani ya mikoa mitatu tofauti.
Mchezo wa mapema zaidi leo ulichezwa mkoani Arusha Kati ya Polisi Tanzania na Mbuni kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid na kumalizika kwa Polisi kuibuka na ushindi wa mabao 2-1.
Mchezo uliosubiriwa kwa hamu zaidi leo Ken Gold dhidi ya Pamba uliopigwa kwenye uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya umemalizika kwa sare ya mabao 2-2 hivyo kila timu kugawana alama na kubaki kwenye nafasi zao.
Mchezo mwengine wa saa 10:00 alasiri Kati ya Copco na Mbeya City kwenye uwanja wa Nyamagana mkoani Mwanza umemalizika kwa sare ya mabao 2-2.