KEN GOLD KINARA WA USHINDI NBC CHAMPIONSHIP.

 

MICHEZO 208 imechezwa ndani ya Ligi ya NBC Championship sawa na michezo 26 kwa kila timu huku jumla ya mabao 490 yakifungwa mpaka sasa.

Ken Gold kinara wa Ligi ya NBC Championship ndio timu iliyoshinda michezo mingi mpaka sasa ikishinda 18 huku ikifunga mabao 44 na kufungwa 15.

Pamba, Biashara na Mbeya Kwanza zinafuatia kila mmoja ikishinda michezo 16 Kati ya 26 iliyocheza mpaka sasa.

Pamba inashika nafasi ya pili ikiwa na alama 55 huku Biashara United na Mbeya Kwanza zikifuatia kila mmoja ikiwa na alama 53 zikitofautiana kwa idadi ya mabao ya kufunga na kufungwa Biashara ikiwa na tofauti ya mabao 29 huku Mbeya Kwanza ikiwa na 17.

Ruvu Shooting ndio timu iliyoshinda michezo michache zaidi ikifanya hivyo mara mbili pekee kwenye michezo 26 iliyocheza mpaka sasa huku ikishika nafasi ya mwisho kwenye Ligi ya NBC Championship.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *